WASHINGTON – Jarida la Marekani la The New Yorker limeripoti kuwa makubaliano yoyote yatakayofikiwa na Donald Trump kwa ajili ya kumaliza mzozo na Iran yatakuwa ya fedheha kwake, kutokana na mazingira magumu aliyoyatengeneza yeye mwenyewe.

Kwa mujibu wa uchambuzi wa chombo hicho cha habari, vita dhidi ya Iran vimegeuka na kuwa “kushindwa kimkakati” kwa upande wa Marekani, huku serikali ya Iran kwa sasa ikijikuta katika nafasi yenye nguvu zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa katika hali ya sasa, Trump amelazimika kufanya maamuzi kati ya chaguo “baya” na “baya zaidi,” na inaonekana wazi kuwa ameelekea kwenye chaguo ambalo ni “baya sana.” Inadaiwa kuwa chini ya mfumo wa makubaliano hayo yaliyopendekezwa, Iran haitapata tu fedha taslimu, bali pia itanufaika na kuondolewa kwa vikwazo vya kiuchumi.

Jarida hilo linahitimisha kwa mtazamo kuwa, vita vilivyoanzishwa kwa lengo la kuiangusha serikali ya Iran, katika uhalisia wake, vimeishia kuipa nguvu na kuiimarisha serikali hiyo zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *