LONDON – Shirika la utangazaji la BBC limeripoti kuwa Urusi imeingilia na kuvuruga mfumo wa mawasiliano wa GPS wa ndege iliyokuwa ikimsafirisha Waziri wa Ulinzi wa Uingereza.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, tukio hili lilitokea mnamo Mei 21, wakati Waziri huyo (Healey) alipokuwa safarini kurejea nchini Uingereza. Awali, waziri huyo alikuwa nchini Estonia ambako alienda kuwatembelea wanajeshi wa Uingereza wanaoshiriki katika mazoezi ya kijeshi ya muungano wa NATO, yaliyokuwa yakifanyika karibu na mpaka wa Urusi.

Inaelezwa kuwa, wakati wa safari hiyo iliyochukua takriban saa tatu, mfumo mkuu wa kuongoza ndege (GPS) ulikata na kushindwa kufanya kazi kabisa. Kufuatia hitilafu hiyo, marubani wa ndege hiyo walilazimika kutumia mfumo mbadala wa uelekeo ili kuhakikisha ndege inafika salama.

Aidha, waandishi wa habari wamebainisha kuwa safari ya ndege hiyo ya serikali haikuwa ya siri, kwani njia iliyokuwa ikipitia ingeweza kufuatiliwa kwa urahisi na mtu yeyote kupitia mitandao ya umma inayoonyesha mienendo ya ndege mtandaoni.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *