Makubaliano ya kusitisha mapigano yameripotiwa kukiukwa na Marekani kufuatia uthibitisho kutoka kwa vikosi vyake kuhusu kutekeleza mashambulizi katika maeneo ya kusini mwa Iran.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Fox News, likinukuu taarifa kutoka Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM), mashambulizi hayo yalilenga maalum vituo vya kurushia makombora pamoja na boti zilizokuwa zikijaribu kutega mabomu (mina) baharini.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Msemaji wa Kamandi Kuu ya Marekani ameeleza kuwa vikosi vyao vilitekeleza mashambulizi hayo siku ya Jumatatu kusini mwa Iran. Hata hivyo, msemaji huyo ametetea hatua hiyo akidai kuwa ilichukuliwa kwa lengo la kujilinda dhidi ya vitisho vya kiusalama.