Umoja wa Ulaya unalazimika kugeukia matumizi ya mbolea ya asili (kinyesi cha wanyama) ili kukabiliana na uhaba mkubwa wa mbolea za kemikali unaolikabili bara hilo. Hali hii inatokana na athari za kiuchumi za vita vinavyoendelea, ambavyo vimevuruga njia kuu za usafirishaji katika Mlango-Bahari wa Hormuz.

Ripoti kutoka shirika la habari la POLITICO zinaeleza kuwa, mzozo kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran umesababisha kusimama kwa takriban theluthi moja ya usambazaji wa mbolea za kemikali duniani, jambo linalotishia usalama wa chakula na sekta ya kilimo barani Ulaya.

Hata hivyo, wataalamu wameonya kuwa suluhisho hili si la kudumu. Herbert Dorfmann, Mbunge wa Bunge la Ulaya (MEP) kutoka Italia, amesema kuwa ingawa mbolea ya wanyama inaweza kutoa msaada wa muda mfupi, haiwezi kuwa mbadala kamili wa mbolea za viwandani kama urea na zile zinazotokana na nitrojeni.

Dorfmann alisisitiza kuwa utegemezi wa muda mrefu wa kinyesi cha ng’ombe pekee hautatosheleza mahitaji makubwa ya wakulima, na hivyo kuibua hofu ya kuendelea kwa changamoto za uzalishaji wa mazao ikiwa hali ya usalama katika njia hiyo ya bahari haitarejea katika hali ya kawaida.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *