Kocha mkuu wa Manchester City, Pep Guardiola, anatarajiwa kuachia ngazi majira ya joto mwaka huu, hatua itakayohitimisha moja ya vipindi vya mafanikio makubwa zaidi katika historia ya Ligi Kuu ya England (Premier League).

Vyanzo mbalimbali vya habari vilivyo karibu na klabu hiyo vinaeleza kuwa, Guardiola anajiandaa kuondoka mwishoni mwa msimu huu ambao tayari kikosi chake kimeshatwaa makombe ya Carabao na FA.

Ushindi wa Jumamosi dhidi ya Chelsea umemhakikishia kocha huyo mwenye umri wa miaka 55 taji lake la 20 kubwa ndani ya kipindi cha miaka 10 aliyodumu kunako dimba la Etihad.

Kufuatia taarifa hizo, aliyekuwa kocha wa Chelsea, Enzo Maresca, anapewa nafasi kubwa ya kwenda kuchukua mikoba ya kuinoa miamba hiyo ya soka. Maresca anatarajiwa kupewa jukumu hilo zikiwa zimepita miezi minne pekee tangu aondoke Chelsea, huku Manchester City ikisalia kwenye nafasi nzuri ya kuweza kutwaa ubingwa mwingine wa Ligi Kuu msimu huu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *