Serikali za India na Falme za Kiarabu (UAE) zimesaini mikataba mipya inayohusu ulinzi na usambazaji wa mafuta ya petroli wakati wa ziara ya kiserikali ya Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, nchini UAE siku ya Ijumaa.

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya India (MEA), makubaliano hayo mapya yanaimarisha zaidi “Ushirikiano Mkakati Kamili kati ya India na UAE” ambao tayari upo kati ya nchi hizo mbili.

Msemaji wa wizara hiyo, Randhir Jaiswal, alisema kuwa ziara hiyo imezaa matokeo saba muhimu. Miongoni mwao ni makubaliano ya ushirikiano kati ya kampuni ya Indian Strategic Petroleum Reserves Limited (ISPRL) na Abu Dhabi National Oil Company (ADNOC).

Mbali na hilo, pande hizo mbili pia zimekubaliana kuanzisha Ushirikiano Mkakati wa Ulinzi pamoja na mpango wa uwekezaji wa maendeleo wenye thamani ya dola bilioni tano kutoka UAE.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *