Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken, amesema kuwa kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Iran ni chagua la makosa, licha ya mjadala uliokuwepo kuhusu hatua hiyo katika serikali mbalimbali za Marekani.

AAkizungumza katika mahojiano ambayo pia yalihudhuriwa na Kansela wa zamani wa Ujerumani, Olaf Scholz, Blinken alisema kuwa suala la kutumia chaguo la kijeshi dhidi ya Iran limekuwa likijadiliwa kwa muda mrefu, hata katika kipindi cha utawala wa Rais wa zamani Barack Obama.

Alieleza kuwa serikali yao ililichunguza kwa makini chaguo hilo, lakini mwishowe ilihitimisha kwamba kutokana na baadhi ya maendeleo na matukio yanayoonekana sasa, hatua ya kijeshi haikuwa njia bora ya kushughulikia suala hilo.Katika mahojiano hayo, Blinken pia alitoa onyo kuhusu kupungua kwa uaminifu wa Marekani miongoni mwa washirika wake wa Ulaya.

Akirejea matokeo ya utafiti mpya wa maoni ya umma, alisema kuwa takribani asilimia 70 ya raia wa Ujerumani sasa wanaiona Marekani kama adui au mshindani badala ya mshirika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *