Ursula von der Leyen amesema kuwa hatua zinachukuliwa dhidi ya TikTok kutokana na muundo wake unaodaiwa kuchochea uraibu kwa watumiaji.
Amesema vipengele kama kuvinjari bila kikomo, video kuchezwa zenyewe, pamoja na arifa za mara kwa mara ni sehemu ya tatizo hilo.
Pia, amesema hatua kama hizo zinaihusu Meta, kwa madai kwamba majukwaa yake ya Instagram na Facebook yanashindwa kutekeleza ipasavyo kiwango cha chini cha umri wa miaka 13 kwa watumiaji wake.
Aidha, von der Leyen amesema kuwa taratibu zimeanzishwa dhidi ya kampuni ya X kufuatia matumizi ya Grok katika kuunda na kusambaza maudhui yanayoonyesha unyanyasaji wa kingono wa watoto.