Mwanastratejia wa Chama cha Democrat, Mike Nellis, amesema sehemu kubwa ya Wamarekani inaonyesha kutoridhishwa na jinsi Ikulu ya Marekani inavyoshughulikia mgogoro wa bei ya mafuta pamoja na upatikanaji wake.
wKwa mujibu wa Nellis, ongezeko la bei ya petroli na chakula limezua hasira miongoni mwa wananchi, huku baadhi wakimlaumu Donald Trump kwa kuanzisha vita vilivyochangia hali hiyo.
Aidha, alibainisha kuwa tafiti za maoni zinaonyesha kushuka kwa kiwango cha umaarufu wa rais. Nellis pia alisema serikali inaonekana kukosa mkakati ulio wazi na kuonyesha hali ya kuchanganyikiwa katika kushughulikia vita dhidi ya Iran.a