Gazeti la Times of Israel limetoa tahariri likikosoa vikali tukio la kufukuliwa kwa kaburi la Mpalestina linalodaiwa kufanywa na walowezi wakiwa chini ya uangalizi wa jeshi la Israel.
Gazeti hilo limeeleza kuwa kitendo hicho kimeibua maswali mazito ya kimaadili ndani ya jamii ya Israel.Kwa mujibu wa tahariri hiyo, tukio hilo lilitokea huku wanajeshi wakiwa karibu na eneo la tukio.
Badala ya kuchukua hatua za kuzuia au kukomesha kitendo hicho, wanajeshi hao waliripotiwa kushuhudia bila kuingilia kati.
Times of Israel imeeleza kuwa vitendo vya aina hiyo haviakisi nguvu, bali vinaashiria changamoto za kimaadili na vinakinzana na misingi ya Kiyahudi ambayo Israel hudai kuilinda.
Gazeti hilo pia limeonya kuwa kuvumilia au kupuuza matukio kama hayo kunaweza kudhoofisha madai ya “tofauti ya kimaadili” ambayo Israel imekuwa ikiyasisitiza kwa muda mrefu.Katika tahariri hiyo, gazeti limehimiza kurejea katika misingi ya haki na huruma, likisema kuwa tabia zinazochukuliwa kuwa za “sumu” zinaweza kuathiri mshikamano na maadili ya jamii kwa ujumla.