Kampuni ya Trump Media and Technology Group, mmiliki wa jukwaa la Truth Social lililoanzishwa na Rais wa Marekani Donald Trump, imeripoti hasara halisi inayozidi dola milioni 400 katika robo ya kwanza ya mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni hiyo, hasara hiyo imetokana na kuporomoka kwa soko la sarafu za kidijitali, hususan Bitcoin, ambalo limeathiri kwa kiasi kikubwa thamani ya uwekezaji wake.

Mwaka mmoja uliopita, kampuni hiyo ilitangaza kukusanya dola bilioni 2.5 kwa lengo la kuwekeza katika sekta ya sarafu za kidijitali, ambayo imekuwa miongoni mwa maeneo yenye kipaumbele kwa Rais Trump katika masuala ya biashara na teknolojia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *