Kituo cha Al-Arabiya kikinukuu chanzo cha serikali ya Pakistan kimeripoti kuwa Rais wa Marekani ameiomba Iran kutoa jibu la haraka kwa pendekezo la amani lililotumwa na Washington. Kwa mujibu wa chanzo hicho, Iran huenda ikawasilisha jibu hilo leo kupitia Serikali ya Pakistan.
Chanzo hicho kimeeleza kuwa mawasiliano kati ya maafisa wa Pakistan na Iran bado yanaendelea bila changamoto yoyote, na kwamba hakuna kikwazo kinachozuia pande hizo mbili kuendeleza mazungumzo au kubadilishana taarifa.
Aidha, katika mazungumzo hayo, chanzo cha Pakistani kimetaja umuhimu wa Mlango Bahari wa Hormuz na kusema kuwa suluhisho la muda mrefu kuhusu eneo hilo nyeti la kimkakati linaonekana kuwa ndani ya uwezo wa kufikiwa.