Israel imeamuru kuondolewa kwa baadhi ya brigedi zake za mapigano kutoka kusini mwa Lebanon kufuatia kuongezeka kwa tishio la mashambulizi ya droni za FPV, kwa mujibu wa Channel 11 ya utawala wa Kizayuni.
Kwa upande mwingine, droni za FPV zinazodaiwa kutumiwa na Hezbollah zimeripotiwa kuonyesha ufanisi katika kushambulia vikosi vya Israel, hata katika maeneo yaliyo nje ya mipaka ya Lebanon.