BANDAR ABBAS, IRAN – Mamlaka katika Mkoa wa Hormozgan imetoa tahadhari kwa wakazi wa mji wa Bandar Abbas kufuatia mipango ya kufanya milipuko iliyodhibitiwa katika maeneo mbalimbali ya mji huo leo Jumapili, Juni 4.
Katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Gavana wa mkoa huo, imeelezwa kuwa sauti kubwa za milipuko zinaweza kusikika, hali inayotokana na operesheni maalum ya kuondoa hatari.
Tunawajulisha wananchi kuwa leo Jumapili, kutakuwa na shughuli ya kutegua na kulipua mabaki ya makombora ambayo hayakulipuka wakati wa mashambulizi ya awali ya Marekani na utawala wa Kizayuni.
Mamlaka hizo zimefafanua kuwa operesheni hiyo ni ya kiusalama na inayodhibitiwa kikamilifu ili kuhakikisha usalama wa raia, huku ikiwataka wakazi wa maeneo husika kutokuwa na hofu pindi watakapoisikia sauti hiyo ya milipuko.