PYONGYANG, KOREA KASKAZINI – Kiongozi Mkuu wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, ametangaza mkakati mpya wa kijeshi unaolenga kuongeza uwezo wa nchi hiyo baharini kupitia ujenzi wa meli kubwa za kivita kwa miaka mitano ijayo.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa meli mpya ya kivita ya tani 5,000 iitwayo Choe Hyon katika bandari ya Nampho, kiongozi huyo ametoa agizo kuwa nchi hiyo inapaswa kujenga meli mbili za aina hiyo kila mwaka. Shirika la Habari la Serikali (KCNA) limeripoti kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kuimarisha ulinzi wa mipaka ya majini.

Katika hotuba yake, Kim alibainisha kuwa jeshi la wanamaji linajiandaa kupeleka meli nyingine ya kivita, Kang Kon, huku kukiwa na mipango ya baadaye ya kuunda meli kubwa zaidi za kimkakati zenye uzito wa hadi tani 10,000.

Mbali na ujenzi wa meli hizo, Kim Jong Un amesisitiza umuhimu wa kuanzisha vituo vipya vya kisasa vya wanamaji. Alieleza kuwa juhudi za kisasa za kijeshi, ikiwa ni pamoja na mpango wa “nyuklia” katika jeshi la wanamaji, zinaendelea kwa kasi kubwa.

Kiongozi huyo alihitimisha kwa kusema kuwa uwezo wa baadaye wa jeshi la wanamaji la Korea Kaskazini utakuwa ni wa “ajabu na usiofikirika,” akiamini kuwa mabadiliko hayo yataifanya nchi hiyo kuwa na nguvu isiyotikisika baharini.

Leave a Reply