Mgombea wa urais wa Ufaransa Jean‑Luc Mélenchon ametoa maoni yake kuhusu Iran na Mlango wa Hormuz. Mélenchon alisema kuwa nchi inapojilinda ina haki ya kutumia mbinu mbalimbali za ulinzi. Alisema kuwa katika hali kama hiyo, mataifa mengine pia yangefanya vivyo hivyo kulinda maslahi yao ya kitaifa.
Akizungumzia suala la Mlango wa Hormuz, alihoji sababu za mataifa ya nje kuingilia eneo hilo, akisema kuwa liko ndani ya mazingira ya kijiografia ya Iran.
Kwa mtazamo wake, Iran haikukurupuka kuufunga mlango huo wa bahari, bali ni baada ya kukakabiliwa na uvamizi kutoka Marekani na Israel.