WASHINGTON — Mbunge wa Marekani kutoka Chama cha Democratic, Ed Case, amesema kuwa jeshi la Marekani lilipoteza angalau ndege 39 wakati wa vita vya siku 40 vilivyohusisha Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Case alitoa taarifa hiyo Jumanne katika kikao cha kamati ya Seneti alipokuwa akimuhoji Afisa Mkuu wa Fedha wa Pentagon, Jay Hurst, kuhusu kiwango cha hasara za kijeshi zilizopatikana katika operesheni hiyo.Akirejelea ripoti ya The War Zone, mbunge huyo alisema kuwa Marekani ilipoteza takriban ndege 39, huku akibainisha kuwa taarifa hiyo ilitolewa karibu mwezi mmoja uliopita.

Aidha, aliitaka Pentagon kueleza iwapo tayari imefanya tathmini ya gharama za muda mrefu za ukarabati na uingizwaji wa vifaa vilivyoharibiwa au kupotea vitani.

Kwa upande wake, Hurst hakutoa takwimu kamili za gharama hizo, akisema Pentagon bado inahitaji kufanya “uchunguzi kamili” kabla ya kutoa makadirio rasmi.“Kuna gharama zinazohusiana na hasara hizo, lakini nitawasilisha majibu kwa maandishi,” alisema Hurst mbele ya kamati hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti ya The War Zone, Jeshi la Anga la Marekani lilifanya karibu safari za ndege 13,000 katika kipindi cha siku 40 za vita dhidi ya Iran.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *