Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema kuwa nchi yake haikuwahi kupanga kupeleka vikosi vya majini katika Mlango wa Hormuz.

Badala yake, amesema Ufaransa ilikuwa inapendekeza ujumbe wa usalama wa kidiplomasia ambao ungefanyika kwa uratibu na Iran.Akizungumza kuhusu hali ya usalama katika eneo hilo, Macron alisisitiza kuwa operesheni za kijeshi za kutumia nguvu kufungua tena mlango huo wa bahari si jambo linalowezekana na zinaweza kuongeza hatari wakati mvutano wa kikanda ukiendelea.

Kwa mujibu wa rais huyo, hatua ya kwanza inapaswa kuwa kusitishwa kwa mapigano, kisha kufanyika mazungumzo ya kimataifa yanayohusisha Iran ili kuhakikisha usafiri wa baharini unakuwa salama.

Mlango wa Hormuz umeathiriwa sana tangu mwishoni mwa Februari 2026 kufuatia mashambulizi na vitisho vinavyohusishwa na uvamizi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran. Ufaransa pamoja na Uingereza zimekuwa zikishinikiza kuanzishwa kwa ujumbe wa ulinzi wa kimataifa utakaotekelezwa baada ya kupungua kwa uhasama, ukihusisha zaidi ya nchi 50 na kutenganishwa na operesheni za kijeshi za vita.

Katika hatua nyingine, Ufaransa ilipeleka kundi la meli za kivita linaloongozwa na meli ya kubeba ndege ya Charles de Gaullekuelekea Bahari Nyekundu mapema Mei 2026 kama sehemu ya mkakati wa kuimarisha usalama bila kuongeza mvutano. Macron pia anatarajiwa kufanya mikutano na washirika kadhaa, wakiwemo India, ili kujadili uwezekano wa mfumo wa kusindikiza meli kwa hiari mara tu mashambulizi yatakapositishwa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *