Washington, D.C. — Kundi la wabunge 30 wa Chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani wameitaka Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kukomesha kile walichokiita “utata wa miongo kadhaa” kuhusu mpango wa silaha za nyuklia wa Israel.

Katika barua rasmi waliyoielekeza kwa wizara hiyo, wabunge hao walisisitiza umuhimu wa uwazi zaidi kuhusu sera ya Marekani kuhusiana na uwezo wa nyuklia wa Israel.

Mbunge wa Kidemokrasia Joaquin Castro wa jimbo la New Hampshire alisema Jumanne, kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti yake, kwamba suala hilo linahitaji mjadala wa wazi, hasa wakati Marekani ikiunga mkono Israel katika mzozo wake na Iran.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wabunge wameibua maswali kuhusu sera ya muda mrefu ya Marekani ya kutotoa maelezo wazi kuhusu uwezo wa nyuklia wa Israel, wakitaka msimamo wa wazi zaidi kutoka kwa serikali ya Washington.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *