Uhuru wa vyombo vya habari duniani umeshuka hadi kiwango chake cha chini zaidi katika kipindi cha miaka 25, kulingana na ripoti ya Reporters Without Borders. Kwa mara ya kwanza, zaidi ya nusu ya nchi duniani zimeainishwa kuwa na hali “ngumu” au “mbaya sana” kwa uandishi wa habari.
Ripoti hiyo inaashiria kuzorota kwa hali ya vyombo vya habari katika maeneo kama Ulaya Mashariki na Mashariki ya Kati, huku nchi kama Urusi na Iran zikiorodheshwa miongoni mwa hatari zaidi kwa waandishi wa habari.
Ripoti hiyo pia inataja hasa vita vya Israel, ikisema kuwa zaidi ya waandishi wa habari 220 wameuawa katika Ukanda wa Gaza tangu Oktoba 2023. Jana, Israel imemwachilia mwandishi wa habari Ali Samoudi baada ya kushikiliwa kwa mwaka mmoja katika magereza ya Israel chini ya kizuizi cha kiutawala.