Mei 16, 2026 — Jeshi la Wanamaji la Marekani limeongeza kwa kiasi kikubwa uwepo wake wa kijeshi katika Bahari ya Arabia, karibu na Iran, kwa kupeleka makundi makubwa ya meli za kivita na wanajeshi.

Miongoni mwa vikosi vilivyopo ni makundi mawili ya meli za kubeba ndege, USS Abraham Lincoln na USS George H.W. Bush, kila moja ikiwa na takribani wafanyakazi 5,500 pamoja na viharibifu (destroyers) vya daraja la Arleigh Burke. Pia kuna kundi la USS Tripoli lenye wanamaji na wanajeshi wa Marine wapatao 3,000 pamoja na meli za msaada.

Ripoti zinaeleza kuwa viharibifu (destroyers) wengine kadhaa wa Marekani pamoja na meli za vita za pwani wanafanya operesheni kwa kujitegemea katika maji ya eneo hilo ili kuimarisha doria na operesheni za majini.

Kwa ujumla, inakadiriwa kuwa takribani wanajeshi 22,000 wa Jeshi la Wanamaji la Marekani wamepelekwa katika maji ya Bahari ya Arabia na maeneo ya karibu na Iran.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *