Zohran Mamdani amesema kuwa mfumuko wa bei nchini Marekani umeongezeka hadi kufikia kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, akieleza kuwa gharama za maisha zimepanda kwa kiasi kikubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo vyakula, mafuta, huduma za afya na usafiri wa anga.

Meya huyo wa New York alihusisha hali hiyo na matumizi makubwa ya fedha za Marekani katika vita vya nje, hususan mvutano unaohusiana na Iran.

Kwa mujibu wake, fedha zinazotumika kugharamia vita nje ya nchi zingeweza kuelekezwa kuboresha maisha ya wananchi wa Marekani na kusaidia kupunguza mzigo wa gharama za maisha.

Mamdani alisisitiza kuwa umefika wakati wa kubadili vipaumbele vya matumizi ya serikali ili kuhakikisha wananchi wanapata maisha bora na yenye heshima.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *