Katika ufichuzi mpya ambao umezua mshituko katika ukanda wa Mashariki ya Kati, gazeti maarufu la Wall Street Journal limeripoti kuwa nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) imekuwa ikitekeleza msururu wa mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika vilivyo na taarifa za ndani, ripoti hiyo inabainisha kuwa moja ya mashambulizi hayo makali yalitekelezwa mwezi Aprili mwaka huu. Shambulio hilo lililenga miundombinu ya Kampuni ya Kusafisha Mafuta ya Lavan (LORC) iliyoko kwenye Kisiwa cha Lavan nchini Iran.

Ingawa UAE imekuwa ikishukiwa kwa muda mrefu kuhusika na oparesheni hizo za kijeshi, ripoti hii ya Wall Street Journal inatoa uthibitisho wa kwanza wa wazi tangu kutokea kwa matukio hayo. Inaripotiwa kuwa Iran ilijibu mapigo wakati huo kwa kushambulia kiwanda kimoja cha kusafisha mafuta nchini Imarati kama sehemu ya kulipiza kisasi.

Hali hii inaashiria kuongezeka kwa mivutano ya siri ya kijeshi kati ya mataifa hayo mawili jirani, jambo ambalo wachambuzi wa mambo wanasema linaweza kuleta athari kubwa katika usalama wa nishati na utulivu wa Ghuba.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *