Waziri Mkuu wa Uingereza amesema kuwa nchi yake haitajiunga katika vita na Iran. Akizungumza kuhusu suala hilo, Keir Starmer alisisitiza kuwa serikali yake haitaruhusu Uingereza kuingia katika mgogoro wa kijeshi na Tehran.

Starmer alieleza kuwa kuingia vitani na Iran kungeilazimu Uingereza kukabiliana moja kwa moja na taifa hilo, jambo ambalo amesema hataliruhusu kutokea.

Aidha, Waziri Mkuu huyo alitangaza kuwa katika mkutano ujao wa Umoja wa Ulaya atawasilisha mwelekeo mpya wa sera kwa Uingereza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *