Taarifa kutoka katika vyombo vya habari zinaonyesha kuwa mamia ya waandamanaji walijitokeza barabarani wakipinga serikali ya Netanyahu, huku vikosi vya usalama vikisimamisha magari ya kupambana na ghasia pamoja na kutumia magari ya kunyunyizia maji kwa ajili ya kuwatawanya.

Katika jiji la Tel Aviv, waandamanaji walikusanyika katika Uwanja wa Habima wakimtuhumu waziri mkuu huyo na baraza lake la mawaziri kwa, kwa madai yao, kushindwa kukabiliana na kundi la Hamas.

Wakati huohuo, mjini Jerusalem inayokaliwa kimabavu, idadi kubwa ya watu ilishiriki maandamano hayo, na kusababisha polisi kuingilia kati kwa kutumia magari ya maji ili kudhibiti umati.

Hadi sasa, hakuna taarifa za majeruhi zilizotolewa, lakini hali ya taharuki imeendelea kushuhudiwa katika maeneo hayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *