Vyombo vya habari vya Kiarabu vimeripoti kuongezeka kwa ununuzi wa ardhi za kilimo kusini mwa Syria unaofanywa na watu wenye uraia wa nchi mbili wanaodaiwa kuwa na uhusiano na mashirika ya Kiyahudi.
Ripoti hizo pia zinataja kuwepo kwa harakati nyingine sambamba, zikiwemo ziara za ujumbe wa Israeli katika maeneo mbalimbali ya Syria pamoja na ununuzi wa baadhi ya maeneo ya zamani ya kijeshi ya Syria. Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mfululizo wa matukio haya unaonekana kuwa na uratibu maalum badala ya kuwa matukio ya bahati nasibu.
Wachambuzi wanasema hatua hizi zinaonekana kuendana na kauli za baadhi ya viongozi wa harakati za ujenzi wa makazi ya walowezi wa Israeli, akiwemo Waziri wa Fedha wa Israel, Bezalel Smotrich, ambaye mara kadhaa amezungumzia wazo la mradi unaojulikana kama “Israel Kubwa”.
Wakati maendeleo haya yakiripotiwa kusini mwa Syria, serikali ya waasi inayoongozwa na al‑Joulani imetajwa na baadhi ya wachambuzi kuwa haijatoa msimamo wa wazi kuhusu suala hilo, huku pia kukiwa na taarifa za kuwepo kwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya upande huo na Israel.