Msemaji wa Makao Makuu ya Khatam al‑Anbiya amesema kuwa Iran itatoa “jibu kali na la kuangamiza” iwapo hatua yoyote ya kijeshi dhidi ya nchi hiyo itafanywa kutoka ardhi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).a
Katika taarifa yake, msemaji huyo alikanusha ripoti iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi ya UAE akidai kuwa katika siku za hivi karibuni vikosi vya jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran havijafanya operesheni yoyote ya makombora au ndege zisizo na rubani dhidi ya UAE.
Alisisitiza kuwa iwapo operesheni kama hiyo ingefanyika, Iran ingeitangaza wazi na bila kusita.Taarifa hiyo pia iliwaonya viongozi wa UAE kwamba nchi yao, kama ardhi ya Kiislamu, haipaswi kuwa kituo au makazi ya vikosi na vifaa vya kijeshi vya Marekani na Israel. Kwa mujibu wa msemaji huyo, hatua kama hizo zinachukuliwa kuwa usaliti dhidi ya ulimwengu wa Kiislamu.
Aidha, msemaji huyo aliitaka UAE kuepuka kile alichokiita “mtego wa Marekani na Wazayuni,” akisema badala ya kuishambulia Iran kupitia propaganda za vyombo vya habari na tuhuma zisizo na msingi, nchi hiyo inapaswa kujiepusha na ushirikiano na mataifa yanayochukuliwa kuwa maadui wa ulimwengu wa Kiislamu.Katika taarifa hiyo, ilielezwa pia kuwa kwa sasa UAE imekuwa moja ya vituo muhimu vya uwepo wa kijeshi wa Marekani na Israel katika eneo la Mashariki ya Kati, jambo ambalo Iran inaliona kuwa chanzo kikuu cha ukosefu wa usalama katika kanda hiyo.
Msemaji huyo aliongeza kuwa Iran imekuwa ikionyesha uvumilivu dhidi ya kile alichokiita propaganda na msaada wa UAE kwa maadui wa Iran na wa ulimwengu wa Kiislamu, akisema hatua hiyo imechukuliwa kwa kuzingatia usalama wa Waislamu wanaoishi katika nchi hiyo.
Hata hivyo, alionya kwamba ikiwa ardhi ya UAE itatumika kufanya mashambulizi dhidi ya visiwa vya Iran, bandari au fukwe zake, Iran itajibu kwa nguvu na hatua ambayo itasababisha majuto