Seneta mwandamizi wa chama cha Democratic kutoka Kamati ya Mahusiano ya Kigeni ya Seneti ya Marekani amepinga madai ya Rais Donald Trump kwamba vita dhidi ya Iran imekamilika.a
Seneta huyo amesema kuwa kauli ya Trump haiwakilishi hali halisi, kwa kuwa maelfu ya wanajeshi wa Marekani bado wako katika hatari katika maeneo mbalimbali ya Mashariki ya Kati.
Aidha, amesisitiza kuwa Trump alianza vita bila idhini rasmi ya Kongresi, na kwamba tangazo la kumalizika kwa vita hiyo halibadilishi ukweli kuhusu hatua zisizo halali zilizochukuliwa awali.