Ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, imelaani vikali kauli ya Meya wa New York, Zohran Mamdani, kufuatia hatua yake ya kusema kuwa anatafakari uwezekano wa kumkamata kiongozi huyo wa Israel pindi atakapohudhuria mkutano ujao wa Umoja wa Mataifa (UN).

Katika mahojiano ya hivi karibuni, Meya Mamdani alibainisha kuwa anashauriana na timu ya wanasheria wa Jiji la New York ili kufahamu mipaka ya mamlaka yake katika kutoa amri kwa jeshi la polisi kumkamata kiongozi wa kigeni, akimrejelea Netanyahu.

Kauli hiyo ya Meya imeibua mvutano wa kidiplomasia, huku ofisi ya Netanyahu ikionekana kuchukulia hatua hiyo kama uchokozi wa kisiasa dhidi ya kiongozi wao.

Leave a Reply