MOSCOW/KYIV — Jitihada za kidiplomasia za kusaka amani katika mzozo unaoendelea kati ya Urusi na Ukraine zimepata pigo kubwa baada ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin, kususia ombi la kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwenzake wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy.
Katika msimamo mkali ambao unazidi kuondoa matumaini ya suluhu ya kidiplomasia, Rais Putin amekaririwa akisema kuwa kwa sasa, hakuna haja ya kufanya mazungumzo hayo, akidai kuwa hayana tija yoyote kwa wakati huu.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya Rais Zelenskyy kuandika barua ya wazi akiomba kukutana na kiongozi huyo wa Urusi ana kwa ana ili kumaliza uhasama. Hata hivyo, majibu ya Moscow yamekuwa ya kukatisha tamaa.