Akijibu uamuzi huo wa Urusi, Rais Zelenskyy amesema kuwa kwa kukataa wito wa mazungumzo, Urusi imeonesha wazi msimamo wake wa kuendeleza mapigano.

“Kwa mara nyingine tena, Urusi imechagua vita badala ya amani,” alisema Zelenskyy katika ujumbe wake, akionyesha masikitiko yake juu ya jinsi juhudi za kusaka suluhu zinavyogonga mwamba.

Uchambuzi wa wachunguzi wa mambo ya kimataifa unaeleza kuwa kukataa huku kwa Putin ni ishara tosha kwamba mvutano kati ya nchi hizo mbili huenda ukachukua muda mrefu zaidi, huku ulimwengu ukiendelea kushuhudia madhara makubwa ya kibinadamu na kiuchumi yanayotokana na mzozo huu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *