Rais Joseph Aoun na Waziri Mkuu Nawaf Salam wametoa shutuma kali dhidi ya Iran kwa kudai kuwa Israel inapaswa kuacha kulipua Lebanon na kuondoa majeshi yake kutoka kusini mwa nchi hiyo.
Wote wawili wanasisitiza kuwa Tehran ndiyo tatizo, kwa sababu ya kutaka makubaliano yao na Marekani yajumuishe pia suala la Lebanon.
Badala yake, uongozi wa Lebanon unatafuta makubaliano ya kurejesha uhusiano wa kawaida (normalisation) na Israel, na unadai kuwa Hezbollah inapaswa kujisalimisha bila masharti na kukabidhi silaha zake, kabla ya Tel Aviv kuondoa majeshi yake katika ardhi inayokaliwa kwa mabavu na kusitisha kampeni yake ya mashambulizi dhidi ya kusini mwa Lebanon.