Mgogoro wa kisiasa wa Senegal umeshika kasi huku Rais wa nchi hiyo Bassirou Diomaye Faye akimteua mchumi Ahmadou Al Aminou Lo katika nafasi ya Waziri Mkuu akichukua nafasi ya Ousmane Sonko aliyefutwa kazi.

Kuteuliwa Ahmadou Al Aminou Lo katika cheo cha Waziri Mkuu kumeshadidisha mpasuko wakati huu ambapo Bunge la Senegal limepanga kupiga kura kwa ajili ya kumrejesha Sonko katika nafasi ya ubunge.

Rais Bassirou Diomaye Faye wa Senegal amemteua Mchumi wa Ngazi ya juu na mfanyakazi wa zamani wa benki Kuu ya nchi hiyo Ahmadou Al Amodou Lo kuwa Waziri Mkuu ikiwa zimepita siku kadhaa baada ya kumfuta kazi mshauri wake wa zamani Ousmane Sonko na kuivunja serikali.

Lo, anayesifiwa kwa utaalamu wake katika mifumo ya kifedha; anachukua madaraka huku Senegal ikiwa imelemewa na mzigo wa deni unaofikia asilimia 132 ya Pato la Taifa na huku IMF ikiwa imesimamisha msaada wa dola bilioni 1.8 kwa nchi hiyo.

Weledi wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa kufukuzwa Sonko katika cheo cha Waaziri Mkuu shakhsia maarufu sana na aliyekuwa na mchango mkubwa katika kuingia mamlakani Rais Faye kunaashiria kupamba moto mvutano wa miezi kadhaa kati ya pande mbili hizo.

Bunge la Senegal leo Jumanne lilipanga kupiga kuhusu kurejeshwa Ousmane Sonko katika nafasi ya Naibu na kumchagua Spika Mpya kufuatia kujiuzulu mshirika wake El Malick Ndiaye.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *