Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kupitia mtandao wake wa Truth Social kwamba Marekani kwa sasa inachunguza na kutathmini uwezekano wa kupunguza idadi ya wanajeshi wake walioko nchini Ujerumani.

Ameongeza kuwa uchunguzi huo unaendelea na kwamba uamuzi wa mwisho kuhusu suala hilo unatarajiwa kutolewa katika muda mfupi.

Awali ya wiki hii Donald Trump alionyesha kuchukizwa na kauli ya Kansela wa Ujerumani, Friedrich, aliyesema kwamba Marekani imedhalilishwa na Iran katika uvamizi wake wa nchi hiyo.