Serikali ya Burkina Faso imetangaza rasmi kukata uhusiano wa kidiplomasia na Ufaransa, hatua inayotarajiwa kubadilisha mwelekeo wa mahusiano ya kisiasa kati ya nchi hizo mbili.
Katika taarifa iliyotolewa na mamlaka za Burkina Faso, serikali imesema uamuzi huo umechukuliwa kutokana na kile ilichokitaja kuwa kutokuheshimiwa kwa kanuni za heshima ya pande zote na madai ya kuingiliwa kwa masuala ya ndani ya nchi hiyo.
Hatua hiyo inaongeza sura mpya katika mvutano uliokuwepo kati ya Ouagadougou na Paris katika kipindi cha hivi karibuni.