LONDON, UINGEREZA – Ulimwengu wa siasa nchini Uingereza umetikisika leo Jumatatu kufuatia Waziri Mkuu Keir Starmer kutangaza rasmi kujiuzulu nyadhifa zake kama Waziri Mkuu na kiongozi wa chama cha Labour.
Katika hotuba ya hisia kali aliyoitoa nje ya makazi yake rasmi ya Downing Street, Starmer amebainisha kuwa ameamua kuachia ngazi na tayari ameweka bayana ramani ya mpito ili kuhakikisha kuwa serikali haiyumbi.
Mpango wa Uteuzi
Akielezea utaratibu wa kufuata, Starmer amesema: “Nitakiomba Kamati Kuu ya Kitaifa ya chama cha Labour (NEC) kuweka ratiba, ambapo mchakato wa uteuzi utaanza tarehe 9 Julai na unatarajiwa kukamilika kabla ya kuanza kwa mapumziko ya kiangazi ya Bunge.”
Waziri Mkuu amesisitiza kuwa, iwapo kutakuwa na ushindani wa kugombea nafasi hiyo, hatua hii itahakikisha kuwa kiongozi mpya anapatikana na kuapishwa kabla ya Bunge kurejea vikao vyake mwezi Septemba.
Hatima ya Uongozi
Licha ya kutangaza nia yake ya kuondoka, Starmer amethibitisha kuwa hatuondoki mara moja. Amesema, “Nitaendelea kushikilia wadhifa wangu kama Waziri Mkuu hadi mchakato wa kuchagua kiongozi mpya utakapokamilika.”
Amehitimisha kwa kutoa ahadi ya kufanya kila linalowezekana ili kuhakikisha kuwa makabidhiano ya madaraka yanafanyika kwa utulivu na utaratibu unaostahili, akiepuka mtafaruku wowote wa kisiasa wakati wa kipindi hiki cha mpito.
Wananchi na wadau wa siasa sasa wanaelekeza macho yao kwa chama cha Labour kuona ni nani atakayechukua mikoba ya kuongoza serikali hii.