JERUSALEM – Katika hatua inayotajwa kuwa ni mabadiliko ya ghafla ya kiusalama, Jeshi la Israel (IDF) limetangaza mipango ya kuanza kupunguza idadi ya vikosi vyake nchini Lebanon.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa chombo cha habari cha Kann, mabadiliko haya yataanza kutekelezwa rasmi kuanzia kesho saa 06:00 asubuhi. Sambamba na uondoaji huu, Kamandi ya Nyumbani (Home Front Command) ya Israel imethibitisha kuondolewa kwa vikwazo vyote vya usalama vilivyokuwa vimewekwa katika makazi ya raia kaskazini mwa nchi hiyo.
Wakati huo huo, ripoti nyeti kutoka Radio ya Jeshi la Israel imedokeza kuwa uamuzi huo si wa bahati mbaya. Ripoti hiyo inadai kuwa shinikizo kubwa kutoka Tehran limezaa matunda, huku kukiwa na taarifa kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, amemuelekeza Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kuamuru uondoaji wa sehemu ya vikosi vya Israel kutoka maeneo ya kusini mwa Lebanon.
Hali ya usalama katika ukanda huo inaendelea kufuatiliwa kwa karibu, huku wachambuzi wakitathmini athari za maelekezo haya mapya kutoka kwa utawala wa Washington na ushawishi wa Iran katika mzozo huu wa muda mrefu.