Photo taken October 27, 2022, Ebola Sudan doctors inside an isolation center together with suspected patients in Mubende, Uganda. Uganda’s health minister Dr. Jane Ruth Aceng,(L) talking to doctors and nurses, working at the isolation center, during their briefing at the Mubende referral hospital, Mubende, Uganda. - Uganda has registered 32 recorded deaths and 115 confirmed cases from an outbreak of the Ebola- Sudan virus. The first death from this outbreak of the Ebola-Sudan strain was announced on 19 September and as yet, there is no vaccine for this strain. (Photo by BADRU KATUMBA / AFP)

Mahakama Kuu ya Kenya imesitisha kwa muda kuanzishwa kituo cha karantini kwa wagonjwa wa Ebola raia wa Marekani, kilichotarajiwa kujengwa nchini humo. Kufuatia uamuzi huo, wakuu wa Marekani wamedai kuwa  watashughulikia hofu ya Wakenya kuhusiana na kituo hicho.

Taarifa ya Jumamosi kutoka Ofisi ya Jeremy P. Lewin, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia Misaada wa Kigeni, imesema: “Tumejulishwa kuhusu hatua ya mahakama nchini Kenya dhidi ya kituo cha kutenga wagonjwa wa Ebola. Tunawasiliana na mamlaka za Kenya na tuna matumaini kuwa tunaweza kutatua pingamizi hiyo.”

Taarifa hiyo ni majibu ya kwanza ya hadharani kutoka Washington tangu Mahakama Kuu ya Kenya isimamishe mpango wa kuanzisha au kuanza kufanya kazi kituo hicho, hadi pale shauri la kikatiba litakaposikilizwa na kuamuliwa.

Jaji Patricia Nyaundi alitoa maagizo hayo Ijumaa baada ya kundi la kutetea haki kupinga mradi huo, likisema kuwa unazua masuala ya kikatiba na ya maslahi ya umma yanayohitaji mapitio ya kimahakama.

Kituo hicho kilichopendekezwa kimeibua mjadala mkali nchini Kenya, kufuatia taarifa kwamba kitatumika kuwashguhulikia raia wa Marekani wanaoweza kuwa wameathiriwa na Ebola wakati wa mlipuko unaoendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, kuwa Marekani haitawaruhusu kuingia nchini humo waathirika au washukiwa wa ugonjwa wa Ebola na kwamba watatibiwa katika nchi nyingine imewakasirisha sana Wakenya wanaoona kwamba nchi yao inatumiwa kama jaa la taka na Marekani.

Wizara ya Afya ya Kenya imeutetea mpango wa kujenga kituo hicho na kusema ni sehemu ya ushirikiano wa kimataifa kuhusu kukabiliana na magonjwa kwa kuzingatia kanuni zote la afya.

Muungano wa Madaktari Kenya (KMPDU) umeitaka serikali iwe na uwazi kamili kuhusu makubaliano yoyote yanayohusiana na kituo hicho kilichopendekezwa, ukisema masuala ya afya ya umma na usalama yanapaswa kujadiliwa wazi kabla ya mpango wowote kama huo kusonga mbele.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *