Maafisa wa kijeshi wa Marekani katika mkutano

WASHINGTON — Mpasuko mkubwa umeibuka ndani ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) kufuatia kuvuja kwa nyaraka za siri zinazofichua upinzani wa ngazi ya juu wa kijeshi dhidi ya kuendeleza operesheni kubwa dhidi ya Iran.

Kwa mujibu wa ripoti ya gazeti la The Washington Post, makamanda wakuu wa Jeshi la Marekani walitoa maonyo rasmi kwa Waziri wa Ulinzi, Pete Hegseth, wakieleza wazi kuwa kuendelea kwa kampeni kubwa za kijeshi dhidi ya Iran kumevuka uwezo wa kiutendaji na “hakiwezi tena kuhimilika.”

Ufichuzi huo umezua taharuki na hasira kubwa ndani ya Pentagon. Msemaji wa wizara hiyo, Sean Parnell, amelaani vikali kitendo hicho akikitaja kuwa ni uhalifu na usaliti wa wazi kwa wanajeshi wa Marekani.

Hatua hii inaweka wazi mzigo mkubwa unaolikabili jeshi la Marekani katika eneo la Asia Magharibi, kuanzia uhaba wa zana, changamoto za kiugavi, hadi mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya kambi zake.

Wachambuzi wanaeleza kuwa mgogoro huu unadhihirisha hofu ya kweli ya makamanda wa kijeshi kuwa kuendelea kushinikiza vita na Tehran kunaweza kuliingiza jeshi la Marekani kwenye mtego wa mzozo usioweza kushindika.

Leave a Reply