Serikali ya Yemen inayoongozwa na Ansarullah imefanikiwa kuchukua udhibiti wa mji wa kimkakati wa bandari wa Mokha, katika operesheni iliyowawezesha kusimamia eneo la takriban kilomita za mraba 2,600 kando ya pwani ya magharibi ya Yemen. Operesheni hiyo imesababisha mabadiliko makubwa katika uwanja wa vita.
Kutekwa kwa Mokha ni hatua muhimu kwa Serikali ya Yemen inayoongozwa na Ansarullah. Mji huu uko umbali wa kilomita 60 pekee kutoka mlango wa Bab al-Mandab, njia nyeti zaidi ya usafirishaji wa meli duniani. Udhibiti huu unawapa nafasi bora ya kijeshi ya kuimarisha uwezo wao wa kusimamia usafiri wa baharini kupitia jeshi la wanamaji lao, jambo linaloashiria mabadiliko ya nguvu katika ukanda huo.
Wachambuzi wanaona kuwa hatua hii inabadilisha mwelekeo wa vita, huku Serikali ya Yemen inayoongozwa na Ansarullah ikionekana kuimarisha nguvu zao kwenye maeneo ya pwani, jambo ambalo bila shaka litaleta mabadiliko katika siasa za kikanda.