Waziri wa Hazina wa Marekani Scott Bessent amesema Rais Donald Trump amekuwa akipiga simu kwa viongozi wa nchi mbalimbali duniani akiwa na maombi maalum kuhusu kusitishwa kwa uhusiano wao na serikali ya Iran.
Bessent amesema Trump anawasiliana moja kwa moja na viongozi hao ili kuwashinikiza kuacha ushirikiano na kile alichokiita “utawala wa Iran.”
“Trump anapiga simu kwa viongozi wa dunia akiwa na maombi maalum ya kusitisha mahusiano yao na utawala wa Iran,” Bessent amesema.
Kauli hiyo inaonyesha kuongezeka kwa juhudi za kidiplomasia za Washington kuongeza shinikizo la kimataifa dhidi ya Tehran baada ya kushindwa kwa uvamizi na mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Tehran.