Je, Karoline Leavitt amekuwa msemaji hasa wa White House, au “sura ya kike” tu iliyokusudiwa kupamba na kufanya sera kali za Trump zionekane kuwa zenye mvuto na kukubalika?

Karoline Leavitt, mwenye umri wa miaka 28, anasema anaondoka katika nafasi yake ya usemaji White House ili kuishi maisha ya utulivu zaidi na watoto pamoja na mumewe mwenye umri wa miaka 60.

Gazeti la The Guardian limeelezea rekodi yake ya kazi kama mkusanyiko wa uongo, madai yasiyo ya kweli na mashambulizi dhidi ya vyombo vya habari, mambo ambayo wakosoaji wanayaona kuwa yanavuka mipaka ya kawaida ya kazi ya uhusiano na umma.

Baadhi ya wakosoaji wanaamini kuwa taswira ya Leavitt, akiwa kijana, mwenye uchangamfu, na wa kike, ilitumika kama pazia laini la kuuza sera ambazo, kwa uhalisia, ziliambatana na vita, mashinikizo na mabavu.

Kwa mtazamo huo, aliitwa “mdoli wa propaganda” na “muuzaji wa simulizi ya Trump”, mtu aliyetumika kubadilisha sura ya mabavu kuwa taswira inayokubalika na vyombo vya habari.

Hata kama anaondoka jukwaani, lakini swali linabakia kuwa: Je, White House itaacha kuchochea vurugu kwa mbinu ya hadaa, au itabuni tu sura nyingine mpya ya kuficha uhalisia wa mambo?

#utaridi #uchambuzi

Leave a Reply